WASANII WANAHITAJIKA

EMAGS

Thursday, April 4, 2013

MSANII WA FILAMU JIJINI ARUSHA AIBUKIA KWENYE MUZIKI WA HIP HOP

Msanii Ray Swing aliyechuchumaa



Msanii wa siku nyingi katika tasnia ya filamu hapa Jijini Arusha ambaye alivuma ipasavyo kwenye filamu ya MATEKA WA KIROHO na kuiwakilisha vyema Jiji la Arusha katika tasnia hiyo ameamua kuingia kwenye muziki wa hip hop.
Msanii huyu anafahamika kwa jina la RAYMOND NGADA a.k.a Ray swing kama anavyojulikana kwenye tasnia ya muziki huo wa kizazi kipya amesema kua wasanii wa hip hop wakae chonjo kwani yeye ni moto wa kuotea mbali.


Hata hivyo hivi karibuni mwandishi wa blog hii alifanikiwa kumuona msanii Ray swing akitumbuiza katika mkutano wa hadhara wa CHADEMA akiimba wimbo wake uliobeba jina la album ya JEMEDARI na wimbo huo ukionekana kumsifia Mbunge wa Arusha Mjini Mh. Gobless Lema na Katibu Mkuu wa CHADEMA Bwana Wilbroad Slaa.


Msanii huyo anayetokea kundi la sanaa la AGESTA ameamua kuingia kwenye muziki kwa sababu ana vipaji vingi na muziki nao ni moja ya kipaji chake alichotunikiwa na Mwenyezi Mungu ili kuiburudisha na kuielimisha jamii.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii msanii huyo amesema ameamua kuachia album yake ya kwanza inayofahamika kwa jina la JEMEDARI na ameamua kuisambaza bure kabisa kwa watanzania wote na hadi sasa ameshasambaza nakala zaidi ya 400 kwa mashabiki wake.
Aidha alipoulizwa kuwa kilichosababisha yeye kuingia kwenye muziki wa hip hop ni kutokana na yeye kuchuja katika tasnia ya filamu  alisema kuwa ameamua kufanya sanaa ya filamu na muziki kwani vyote anaviweza na anaamini vitamuingizia kipato na kumnyanyua kimaisha.
Ukitaka kumsikiliza au ku-download nyimbo zake zote za album ya JEMEDARI unaweza kuipata bure kabisa kwa kutembelea www.nellykivuyo.blogspot.com sasa ili umpe-support msanii huyu.

Wednesday, April 3, 2013

VIKUNDI VYA SANAA ARUSHA VYAKUTANA ILI KUUNDA UMOJA WAO

Kutoka kushoto ni Ndugu Ray kutoka kikundi cha AGESTA ambaye alikua katibu wa kikao na upande wa kulia ni Bwana Elias Mages Mkurugenzi wa Emags ambaye ndiye aliyekua Mwenyekiti wa kikao hicho


Viongozi mbalimbali wa vikundi vya sanaa ya Filamu na maigizo Jijini Arusha wamekutana jumatatu ya pasaka kwa ajili ya kutathmini mustakabali wa sanaa ya Jijini Arusha kwa kile wanachoeleza kuwa imekosa mwelekeo.
Blog hii ya Arusha Professional Movies ilishuhudia viongozi mbalimbali wa vikundi vya sanaa wakijadili kwa uchungu sanaa yao ambayo imeonekana kupoteza dira kwa kile  wanachoeleza kuwa waliochangia kudidimiza sanaa hiyo ni viongozi wa shirikisho la sanaa lililoundwa mwaka jana kinyemela.
Mmoja wa wajumbe akitoa maoni yake

Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi mdogo wa mikutano wa Kampuni ya Emags Video Entertainment maeneo ya Ilboru tank la maji.
Vikundi vilivyohudhuria kikao hicho ni pamoja na AGESTA, NGURUMO YA UPAKO (NYU), FIRE PLACE, KILELE, EMAGS,OSG,GQ FILMS,FICUS,OLERIEN na vingine vingi.

Isack toka OSG naye alitoa maoni yake

Hata hivyo kwa mujibu wa waandaji wa kikao hicho wamesema kuwa walikuwa wamewaalika viongozi wa shirikisho la sanaa Arusha wakiongozwa na mwenyekiti wao Bw Kassim Digiga ila cha kushangaza viongozi hao waliamua kuandaa Bonanza la wasanii wa filamu na waandishi wa habari ili waharibu kikao ambacho kinalenga kuwang’oa madarakani kwa kile kinachodaiwa hamna wanachokifanya kuinua sanaa ya Arusha zaidi ya kujinufaisha wao wenyewe na familia zao.

Mr Hondohondo naye alitoa yake ya moyoni

“Mimi nawashangaa hawa eti wanajiita viongozi wa shirikisho, kwanza hawana elimu yoyote ya uongozi, wengine wanajiita ma-director na ma-producer lakini hawajui hata camera inapigwaje au inashikwaje” hawastahili kutuongoza alisikika kiongozi mmoja wa kikundi ambaye hakupenda atajwe jina lake.
Teacher KT naye alikuwepo katika kikao hicho

Hata hivyo mwingine aliyejitambulisha kwa jina la HondoHondo alisema kuwa “baadhi ya viongozi wa vikundi wanaanzisha vikundi ili wapate wasichana wa kufanya nao ngono”
Kelvin au Abby toka Emags naye alitoa maoni yake katika kikao hicho

Kikao hicho kilijadili kuanzisha chama mbadala cha kuinua sanaa ya Arusha mwelekeo wa sanaa ya Filamu, usambazaji wa kazi za wasanii, ushirikiano wa vikundi na kama kuna uhalali wowote wa shirikisho la sanaa Arusha na kuwaita viongozi hao wa shirikisho ili wawaeleze jinsi walivyoididimiza sanaa ya filamu Jijini Arusha.

PICHA ZA MATUKIO YA KIKAO HIZI HAPA

Fredy, sophia na mwijage pia walikuwepo