Msanii Ray Swing aliyechuchumaa |
Msanii
wa siku nyingi katika tasnia ya filamu hapa Jijini Arusha ambaye alivuma
ipasavyo kwenye filamu ya MATEKA WA KIROHO na kuiwakilisha vyema Jiji la Arusha
katika tasnia hiyo ameamua kuingia kwenye muziki wa hip hop.
Msanii
huyu anafahamika kwa jina la RAYMOND NGADA a.k.a Ray swing kama anavyojulikana
kwenye tasnia ya muziki huo wa kizazi kipya amesema kua wasanii wa hip hop
wakae chonjo kwani yeye ni moto wa kuotea mbali.
Hata
hivyo hivi karibuni mwandishi wa blog hii alifanikiwa kumuona msanii Ray swing
akitumbuiza katika mkutano wa hadhara wa CHADEMA akiimba wimbo wake uliobeba
jina la album ya JEMEDARI na wimbo huo ukionekana kumsifia Mbunge wa Arusha
Mjini Mh. Gobless Lema na Katibu Mkuu wa CHADEMA Bwana Wilbroad Slaa.
Msanii
huyo anayetokea kundi la sanaa la AGESTA ameamua kuingia kwenye muziki kwa
sababu ana vipaji vingi na muziki nao ni moja ya kipaji chake alichotunikiwa na
Mwenyezi Mungu ili kuiburudisha na kuielimisha jamii.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hii msanii huyo amesema ameamua kuachia album yake ya
kwanza inayofahamika kwa jina la JEMEDARI na ameamua kuisambaza bure kabisa kwa
watanzania wote na hadi sasa ameshasambaza nakala zaidi ya 400 kwa mashabiki
wake.
Aidha
alipoulizwa kuwa kilichosababisha yeye kuingia kwenye muziki wa hip hop ni
kutokana na yeye kuchuja katika tasnia ya filamu alisema kuwa ameamua kufanya sanaa ya filamu
na muziki kwani vyote anaviweza na anaamini vitamuingizia kipato na kumnyanyua
kimaisha.
Ukitaka
kumsikiliza au ku-download nyimbo zake zote za album ya JEMEDARI unaweza
kuipata bure kabisa kwa kutembelea www.nellykivuyo.blogspot.com sasa ili
umpe-support msanii huyu.