KASSIM a.k.a KIM |
Katika
hali isiyokuwa ya kawaida na yakushangaza,wasanii wa filamu waliokuwa wameweka
kambi kwaajili ya kurekodi filamu ambayo bado haijapewa jina kamili,wakiwa
katika maeneo ya Esso jijini Arusha,wamejikuta katika hali yamdomo wazi baada
ya kutimuliwa katika kambi hiyo hivi karibuni kwa kile kinachodaiwa kukithiri
kwa vitendo vya ngono ndani ya kambi hiyo.
Kwa
habari kamili zilizofikia meza ya habari ya blog hii na kuzibitishwa na
mwenyekiti wa shirikisho la sanaa ya filamu jiji la Arusha Bw.Kassim maarufu
kwa jina la Kim,zilidai kuwa kambi hiyo ilikuwa inatia kichefuchefu na kukosa
maadili ya sanaa.
“Ndugu
mwandishi yani huwezi kuamini,mimi nilipata habari hizi kupitia mmoja wa
wasanii na ikanilazimu kama kiongozi niende katika hiyo kambi iliyokuwa maeneo
ya Eso nakushuhudia madudu hayo ,kama mwenyekiti niliamua kuivunja na kuwatimua
wasanii wote na kuwaambia kama wataendelea nitaita polisi,sasa cha kushangaza
aliyekuwa anaongoza kambi hiyo ni kiongozi mmoja wa ngazi ya juu katika
shirikisho(jina kapuni)”.alinukuliwa Bw.Kim akisema.
Baada
ya kubanwa kwa muda mwenyekiti aliamua kufunguka juu ya kiongozi huyo kuwa ni
katibu wa shirikisho hilo Bw.Isack ambaye inasemekana amejiuzuru katika wazfa
huo baada ya mtafaruku baina ya viongozi kisa pesa.
Aidha
wasanii hao walidaiwa kukesha kambini hapo huku kila mtu akiwa na mwenza wake
ndani ya wasanii hao hao na hata muda mwingine kubadilishana bila hata
uwoga wala aibu.
Kwa
niaba ya wanasanaa,dawati la habari la blog hii linawaomba wasanii kujiheshimu
na pia kwa wale ambao wanavamia sanaa na kuitia doa kuacha kwani sanaa ni kazi
na si mahali pakufanyia uhuni.
No comments:
Post a Comment