MWANAHAMISI MZIRAY a.k.a MISHI |
Mwanadada
machachari aliyeuza sura nakufanya vema katika filamu bomba ya Standard 7
Mwanahamisi Mziray kwa jina maalufu “Mishi” ametimiza usemi wa filamu hiyo
baada ya kukimbia kupiga kitabu katika vyuo viwili tofauti mkoani hapa.
Mrembo
huyo alikuwa akipiga darasa katika chuo cha Sila huku akisoma ishu za mapishi
nakujikuta akiingia katika kisanga hicho baada yakunogewa na uuzaji sura .
Hata
hivyo baada ya kumaliza filamu hiyo alipata shavu kubwa lingine lakuigiza filamu iliyotumia lugha
yakimombo nakujikuta akitupilia mbali
ishu ya kupika na kukimbilia katika chuo maarufu cha lugha jina tunalihifadhi
nakuanza kujifunza lugha hiyo.
Aidha
alijikuta katika wakati mgumu baada ya muda aliopewa na waandaaji wa filamu
hiyo toka nchini Kenya kuisha huku kimombo kikiwa bado cha yes/no??!!”? ,hali
iliyopelekea msanii huyo kukimbia tena daftali nakufanya filamu zenye lugha ya
Kiswahili.
Baada
yakupoteza bahati hiyo,alipotezea ishu za kitabu nakuamua kulandalanda akisaka
filamu za kucheza kujiwekea jina hata kama ni bure jambo ambalo lilizidi
kumpoteza kabisa katika tasnia hiyo licha yakufanya vema katika filamu ya
standard 7.
Baada
ya kudakishwa kwa stori hii,blog hii ilimlushia waya Mishi naye alikiri
kukimbia kitabu lakini si kwakutopenda kitabu bali mikataba mingi ya kucheza
filamu ndani na nje ya Arusha hivyo hali hiyo kumpa ugumu wakutulia kusoma
labda kwa baadae sana.
MISHI |
No comments:
Post a Comment