Kutoka kushoto ni Ndugu Ray kutoka kikundi cha AGESTA ambaye alikua katibu wa kikao na upande wa kulia ni Bwana Elias Mages Mkurugenzi wa Emags ambaye ndiye aliyekua Mwenyekiti wa kikao hicho |
Viongozi
mbalimbali wa vikundi vya sanaa ya Filamu na maigizo Jijini Arusha wamekutana
jumatatu ya pasaka kwa ajili ya kutathmini mustakabali wa sanaa ya Jijini
Arusha kwa kile wanachoeleza kuwa imekosa mwelekeo.
Blog
hii ya Arusha Professional Movies ilishuhudia viongozi mbalimbali wa vikundi
vya sanaa wakijadili kwa uchungu sanaa yao ambayo imeonekana kupoteza dira kwa
kile wanachoeleza kuwa waliochangia
kudidimiza sanaa hiyo ni viongozi wa shirikisho la sanaa lililoundwa mwaka jana
kinyemela.
Mmoja wa wajumbe akitoa maoni yake |
Hata
hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi mdogo wa
mikutano wa Kampuni ya Emags Video Entertainment maeneo ya Ilboru tank la maji.
Vikundi
vilivyohudhuria kikao hicho ni pamoja na AGESTA, NGURUMO YA UPAKO (NYU), FIRE
PLACE, KILELE, EMAGS,OSG,GQ FILMS,FICUS,OLERIEN na vingine vingi.
Isack toka OSG naye alitoa maoni yake |
Hata
hivyo kwa mujibu wa waandaji wa kikao hicho wamesema kuwa walikuwa wamewaalika
viongozi wa shirikisho la sanaa Arusha wakiongozwa na mwenyekiti wao Bw Kassim
Digiga ila cha kushangaza viongozi hao waliamua kuandaa Bonanza la wasanii wa
filamu na waandishi wa habari ili waharibu kikao ambacho kinalenga kuwang’oa
madarakani kwa kile kinachodaiwa hamna wanachokifanya kuinua sanaa ya Arusha
zaidi ya kujinufaisha wao wenyewe na familia zao.
Mr Hondohondo naye alitoa yake ya moyoni |
“Mimi
nawashangaa hawa eti wanajiita viongozi wa shirikisho, kwanza hawana elimu
yoyote ya uongozi, wengine wanajiita ma-director na ma-producer lakini hawajui
hata camera inapigwaje au inashikwaje” hawastahili kutuongoza alisikika kiongozi
mmoja wa kikundi ambaye hakupenda atajwe jina lake.
Teacher KT naye alikuwepo katika kikao hicho |
Hata
hivyo mwingine aliyejitambulisha kwa jina la HondoHondo alisema kuwa “baadhi ya
viongozi wa vikundi wanaanzisha vikundi ili wapate wasichana wa kufanya nao
ngono”
Kelvin au Abby toka Emags naye alitoa maoni yake katika kikao hicho |
Kikao
hicho kilijadili kuanzisha chama mbadala cha kuinua sanaa ya Arusha mwelekeo wa
sanaa ya Filamu, usambazaji wa kazi za wasanii, ushirikiano wa vikundi na kama
kuna uhalali wowote wa shirikisho la sanaa Arusha na kuwaita viongozi hao wa
shirikisho ili wawaeleze jinsi walivyoididimiza sanaa ya filamu Jijini Arusha.
PICHA ZA MATUKIO YA KIKAO HIZI HAPA
Fredy, sophia na mwijage pia walikuwepo |
Mm n binti wa miaka 22 naishi Arusha mjn napenda filamu sana na napenda kuigiza je ntawezaje kijiunga na vikundi vya filamu please 🙏
ReplyDelete