WASANII WANAHITAJIKA

EMAGS

Tuesday, February 26, 2013

WASANII WA FILAMU WAJITOSA SHINDANO LA THE YOUNG MILLIONAIRE REALITY TV SHOW KUWANIA TSH 10,000,000




Lile shindano la kumtafuta kijana mwenye kipaji cha ujasiriamali linaloendeshwa na kampuni mahiri ya kutengeneza filamu, documentary na upigaji picha wa aina zote za video ya Emags Video Entertainment iliyopo Jijini  Arusha litakaloanza kurushwa hivi karibuni kupitia Televisheni ya Taifa (TBC1) limeingiliwa.

Habari za uhakika toka kampuni ya Emags Video Entertainment zinasema kuwa shindano hilo litaanza kurushwa hivi karibuni na washiriki wanaendelea kujisajili kwa wale wa mkoa wa Arusha tu.
Katika kuonesha vipaji vyao vya ujasiriamali, wasanii pia nao wameamua kuingia katika kinyang’anyiro hicho cha kugombea shilingi 10,000,000 (milioni kumi za kitanzania). Wasanii hao waliochukua fomu ni pamoja na 

Mwanahamisi Mziray a.k.a Mishy
Fred Kadege
Charles Mwise
Abby Carter na
Lilian Urassa
Pia akizungumza na mwandishi wetu Afisa Uhusiano wa kampuni ya Emags Video Entertainment ndugu Severinus Mwijage Jr amesema “Kwa sasa tuna mshukuru Mungu tumemaliza usahili katika mikoa mbalimbali kama Mwanza, Kagera, Morogoro, Dodoma, Musoma, Kilimanjaro, Tanga na Manyara”

Aliongeza pia “Mkoa wa Arusha ndio tunafanya mchakato wa kupata washiriki, kwa wale wanaotaka kushiriki shindano hili wafike katika ofisi zetu zilizopo tank la maji Ilboru Jijini Arusha kwani nafasi zipo chache”

Afisa Uhusiano huyo aliendelea kusema kuwa “ Ndugu mwandishi tunavyozungumza sasa tumetoka katika hoteli ya PENGUIN RESORT HOTEL iliyopo Sakina Jijini Arusha na tumezungumza na Meneja wao na wametoa ruhusa ya shindano hili kufanyika katika hoteli yao, tunawashukuru sana uongozi wa PENGUIN RESORT HOTEL kwa kukubali kuinua vipaji vya vijana katika Nyanja ya ujasiriamali”
Blog hii inawatakia kila la kheri wasanii hao ili waweze kufikia malengo yao.

Kwa wale wanaotaka kushiriki shindano hili la THE YOUNG MILLIONAIRE REALITY TV SHOW wenye umri kati ya miaka 18 hadi 30 unaweza kuwasiliana na Emags Video Entertainment kupitia namba zifuatazo

+255 754 014 227                                    
+255 656 396 025


Monday, February 25, 2013

NGONO ZEMBE YAVURUGA KAMBI YA WASANII

KASSIM a.k.a KIM


Katika hali isiyokuwa ya kawaida na yakushangaza,wasanii wa filamu waliokuwa wameweka kambi kwaajili ya kurekodi filamu ambayo bado haijapewa jina kamili,wakiwa katika maeneo ya Esso jijini Arusha,wamejikuta katika hali yamdomo wazi baada ya kutimuliwa katika kambi hiyo hivi karibuni kwa kile kinachodaiwa kukithiri kwa vitendo vya ngono ndani ya kambi hiyo.

Kwa habari kamili zilizofikia meza ya habari ya blog hii na kuzibitishwa na mwenyekiti wa shirikisho la sanaa ya filamu jiji la Arusha Bw.Kassim maarufu kwa jina la Kim,zilidai kuwa kambi hiyo ilikuwa inatia kichefuchefu na kukosa maadili ya sanaa.

“Ndugu mwandishi yani huwezi kuamini,mimi nilipata habari hizi kupitia mmoja wa wasanii na ikanilazimu kama kiongozi niende katika hiyo kambi iliyokuwa maeneo ya Eso nakushuhudia madudu hayo ,kama mwenyekiti niliamua kuivunja na kuwatimua wasanii wote na kuwaambia kama wataendelea nitaita polisi,sasa cha kushangaza aliyekuwa anaongoza kambi hiyo ni kiongozi mmoja wa ngazi ya juu katika shirikisho(jina kapuni)”.alinukuliwa Bw.Kim akisema.
Baada ya kubanwa kwa muda mwenyekiti aliamua kufunguka juu ya kiongozi huyo kuwa ni katibu wa shirikisho hilo Bw.Isack ambaye inasemekana amejiuzuru katika wazfa huo baada ya mtafaruku baina ya viongozi kisa pesa.

Aidha wasanii hao walidaiwa kukesha kambini hapo huku kila mtu akiwa na mwenza wake ndani ya wasanii hao hao na hata muda mwingine kubadilishana bila hata uwoga  wala aibu.
Kwa niaba ya wanasanaa,dawati la habari la blog hii linawaomba wasanii kujiheshimu na pia kwa wale ambao wanavamia sanaa na kuitia doa kuacha kwani sanaa ni kazi na si mahali pakufanyia uhuni.