Lile shindano la kumtafuta kijana mwenye kipaji cha
ujasiriamali linaloendeshwa na kampuni mahiri ya kutengeneza filamu,
documentary na upigaji picha wa aina zote za video ya Emags Video Entertainment
iliyopo Jijini Arusha litakaloanza
kurushwa hivi karibuni kupitia Televisheni ya Taifa (TBC1) limeingiliwa.
Habari za uhakika toka kampuni ya Emags Video
Entertainment zinasema kuwa shindano hilo litaanza kurushwa hivi karibuni na
washiriki wanaendelea kujisajili kwa wale wa mkoa wa Arusha tu.
Katika kuonesha vipaji vyao vya ujasiriamali,
wasanii pia nao wameamua kuingia katika kinyang’anyiro hicho cha kugombea
shilingi 10,000,000 (milioni kumi za kitanzania). Wasanii hao waliochukua fomu
ni pamoja na
Mwanahamisi Mziray
a.k.a Mishy
Fred Kadege
Charles Mwise
Abby Carter na
Lilian Urassa
Pia akizungumza na mwandishi wetu Afisa Uhusiano wa
kampuni ya Emags Video Entertainment ndugu Severinus Mwijage Jr amesema “Kwa
sasa tuna mshukuru Mungu tumemaliza usahili katika mikoa mbalimbali kama
Mwanza, Kagera, Morogoro, Dodoma, Musoma, Kilimanjaro, Tanga na Manyara”
Aliongeza pia “Mkoa wa Arusha ndio tunafanya
mchakato wa kupata washiriki, kwa wale wanaotaka kushiriki shindano hili wafike
katika ofisi zetu zilizopo tank la maji Ilboru Jijini Arusha kwani nafasi zipo
chache”
Afisa Uhusiano huyo aliendelea kusema kuwa “ Ndugu
mwandishi tunavyozungumza sasa tumetoka katika hoteli ya PENGUIN RESORT HOTEL
iliyopo Sakina Jijini Arusha na tumezungumza na Meneja wao na wametoa ruhusa ya
shindano hili kufanyika katika hoteli yao, tunawashukuru sana uongozi wa
PENGUIN RESORT HOTEL kwa kukubali kuinua vipaji vya vijana katika Nyanja ya
ujasiriamali”
Blog hii inawatakia kila la kheri wasanii hao ili
waweze kufikia malengo yao.
Kwa wale wanaotaka kushiriki shindano hili la THE
YOUNG MILLIONAIRE REALITY TV SHOW wenye umri kati ya miaka 18 hadi 30 unaweza
kuwasiliana na Emags Video Entertainment kupitia namba zifuatazo
+255 754 014 227
+255 656 396 025