-Amnunulia
lunch kwa kumrubuni
MPENZI WA MWIJAGE WA ZAMANI |
Lile
sakata liliosababisha msanii wa filamu hapa Jijini Arusha kutoka kimapenzi na
wasichana tofauti tofauti limechukua sura mpya baada ya mpenzi wake
aliyemsababishia hiyo hali kutaka kurudisha mahusiano yao ya awali.
SEVERINUS MWIJAGE Jr |
Blog
hii imepata taarifa hizi kupitia msanii huyo ambaye alifunguka baada ya taarifa
hizi kufikia chumba chetu cha habari mapema jana mchana majira ya saa saba.
“Ni
kweli ndugu mwandishi jana majira ya saa saba mchana nilipokea simu kutoka kwa
mpenzi wangu wa zamani ambaye alisema anataka kuzungumza nikamkubalia kwa kuwa
sina ugomvi nae” alisema msanii huyo.
MWIJAGE NA MPENZI WAKE ENZI ZA MAPENZI YAO |
Msanii
huyo anayefahamika kwa jina laSeverinus Mwijage Jr maarufu kama Dj Angwisa aliendelea
kufunguka kuwa “ Binti huyo baada ya kutaka kukutana na mimi alinipeleka kwenye
moja ya mgahawa hapa Mjini akaninunulia chakula cha mchana kwa lengo la kutaka
kunishawishi ili nirudiane nae”
HAPA WALIKUA MOJA YA FUKWE HAPA NCHINI |
Habari
za uhakika zilizopatikana zinasema kuwa binti huyo kwa sasa anahangaika kila
kukicha kutafuta ndugu, jamaa na marafiki wa karibu wa Mwijage ili waweze
kumshawishi kurudisha uhusiano wao wa mwanzo.
MAPENZI YALIKUA MOTOMOTO KWELI ENZI HIZO |
Rafiki
wa karibu wa ndugu Mwijage aliweza kutupenyezea habari kuwa majira hayo ya
mchana binti huyo alionekana nyumbani kwa Mwijage akilazimisha uhusiano wao
kurudia kama zamani lakini ndugu Mwijage alikua na msimamo kuwa hamtaki na hayo
mambo kwa sasa yanazungumzwa kifamilia.
NANI ALIJUA KUWA WATAGOMBANA? |
Endelea
kutembelea blog hii ili tukuhabarishe kitakachoendelea baada ya familia hizi
mbili kuzungumza na binti huyu kuendelea kutafuta muafaka wa penzi lake kwa
Mwijage.
No comments:
Post a Comment