WASANII WANAHITAJIKA

EMAGS

Tuesday, March 19, 2013

BAADA YA KUKIMBIA DARASA NA KUIBUKIA KATIKA TASNIA YA FILAMU. FIGA MAUZO YAJIKUTA YAANGUKIA KATIKA UPISHI WA CHAKULA KATIKA KAMBI YA WASANII.



Baada ya kuanikwa wazi juu ya kukimbia darasa kwa mrembo mwenye figa matata  katika tasnia ya filamu jijini Arusha  Mwanahamisi Mziray (Mishi),bidada huyo amejikuta akizidi kuangukia pua baada ya mambo katika tasnia hiyo kuzidi kumuendea vibaya na kujikuta akiwapikia wenzake chakula katika kambi waliokuwa wameweka kabla ya kuanza kupiga kizigo cha filamu yenye utata hadi hivi sasa.
Bishosti huyo alieonekana kuja kwa kasi katika tasnia hii akiamini ni njia rahisi zaidi ya kutokea mambo yamezidi kumuendea ndivyo sivyo nakujikuta akitapatapa katika vikundi.


Chanzo chetu makini kilitupitishia kavu kavu kuwa bidada Mishi baada ya kuanza vyema kwa kucheza katika filamu ya Standard 7 alijikuta katika wakati mgumu baada ya kuibuka kwa shosti mwingine katika kampuni aliyoanza nayo nakufunikwa katika uchezaji,jambo lililomfanya ahame kampuni nakuanza kusaka vikundi vya sanaa.
Hata hivyo kama ulivyo msemo wa maisha ni popote,Mishi aliamua kutumia swaga hizo na kuanza kusaka sanaa kona hadi kona akiambulia kucheza filamu zisizo isha na kujikuta katika kambi ya kundi la OSG lililokuwa likijianda na kucheza filamu nayeye kujikuta akipewa kazi yakuwapikia wasanii wenzake hata hivyo alifanya akiamini atapata nafasi yakucheza filamu.
Aidha msemo wa kifo cha nyani miti yote kuteleza nao ukadhihilika wazi baada ya bidii yote ya kuwapikia wenzake akisaka nafasi kutokana na wasanii kuwa wengi,kambi hiyo ilivunjwa mara kwa mara kutokana na sababu tofautitofauti ikiwemo ngono nzembe baina ya wasanii nakupelekea kufukuzwa nawahusika wa maeneo waliokuwa wanaweka kambi.
Baada ya kashkash hizo,hakuonekana kukata tamaa akijaribu kusikiza msemo wa penYe nia pana njia lakini mambo hayajaonekana kuwa sawia,hata hivyo blog hii ilizungumza na baadhi ya wasanii wenzake waliokuwa nae kampuni kipindi cha filamu ya standard 7 na kumshauri bidada huyo kutokuogopa chalenji hivyo arudi atulie katika kampuni kwani anazidi kuchuja na kupotea kabisa katika tasnia ya filamu.

No comments:

Post a Comment