JUMAMOSI HII WABABE WA SOKA KAMPUNI YA EMAGS
VIDEO ENTERTAINMENT DIMBANI TENA.
Baada
ya mechi mfululizo za kujiweka fiti kiafya na kudumisha urafiki baina ya makampuni
na vikundi vya sanaa jijini Arusha ,kampuni inayokuwa gumzo mjini Arusha kwa
kazi safi za filamu pamoja na kusakata kabumbu,jumamosi hii tena kuumana na
kundi la sanaa la AYSAG la mjini hapa katika uwanja wa shule ya msingi meru
walio na hamu ya kuonja shubiri ya magoli.
Akizungumza
na blog hii mkurugenzi wa kampuni babkubwa ya filamu jijini hapa Bw : Elias
Magesa ambaye pia ni straika matata afungae dakika za lala salama na kuzua
kilio kwa timu pinzani alisema kampuni yake iko fiti kwa mchezo kwani licha ya
mazoezi ya sanaa kila siku huanza na mazoezi ya viungo jambo linalowaweka
katika ubora kimwili nakuwa tishio katika makampuni na vikundi vya sanaa.
Hata
hivyo amewaomba wasanii wa AYSAG kujipanga vema nakufanya mchezo wa kiungwana
kwa lengo la umoja wavikundi na sio kuweka mamluki kama walivyo fanya kundi la
OSG kwani si lengo la kisanaa na mchezo kwa ujumla,pia aliomba wadada wa kundi
hilo kujitokeza kucheza pia ili soka kuwa nzuri na yenye kuvutia kwa lengo la
furaha.
Nae
mkurugenzi wa kundi la AYSAG Bw: Kim alisema wapo tayari kwa mchezo huo na
kuahidi kuweka wadada ili kuwafanya wasanii wote kushiriki vema katika mchezo
huo kwani hakutakuwa na mchezo wa pete nakuahidi mchezo wakiungwana na furaha
akisema wanajua maana ya michezo na sanaa.
Nae
Kapteni wa timu ya Kampuni ya Emags Ibrahim Jamal amewaomba wasanii wote kuwahi
uwanjani ili kuanza mapema na kuhitimisha kwa furaha za kisanaa,akitoa angalizo
la AYSAG kuwa makini kwani wataondoka na kapu la mabao na kuomba wadau
kujitokeza kushuhudia kandanda safi.
Aidha
blog hii inawatakia mchezo mwema na wenye furan a amani na pia kuahidi kuwapa
wasomaji matokeo kila baada ya dakika ya mchezo huo.
No comments:
Post a Comment