|
KIKOSI CHA MAUAJI CHA EMAGS |
Wasanii
wa filamu kutoka kampuni ya Emags Video Entertainments mwishoni mwa wiki
waliwafundisha mamluki wa kikundi cha OSG
soka la kiulaya na kuwaacha mashabiki wakinongóna wakiifananisha timu
hiyo na timu za ligi kuu bara, na zile za ulaya kwa kiwango walicho kionesha.
|
IBRAHIM JAMAL AKIINGIA UWANJANI |
|
RODGERS AKIWAITA WACHEZAJI KUFANYA WARM UP |
Mechi
hiyo iliyokuwa imejaa kila aina ya mbwembwe za kisanii na majigambo toka kwa
viongozi na mashabiki wa timu hizo hususani mabinti waliokuwa wamefulika katika
kiwanja cha shule ya msingi meru,kilishuhudia kipute hicho kikikamilika kwa
pacha ya goli nne kwa nne licha ya kucheza dakika zaidi ya tisini kwa utashi wa refa aliokuwa
akiwatafutia goli OSG waliokuwa nyuma kwa mabao 4 kwa 3 hadi dakika tisini.
Kuonyesha
kuegemea upande mmoja mwamuzi wa mchezo huo aligomea goli la tano la Emags
baada ya shuti kali lililopigwa na kiungo mchezeshaji wa emags Mau na kumshinda
kipa wa OSG na refa kulikataa akidai hakuwa ameruhusu mpira kuanza.
Naye
mkurugenzi wa OSG bwana Isack aliyejigamba kushinda mechi hiyo kutokana na kuwa
na mamluki wanaocheza ligi ya wilaya Arusha alijikuta akikaa chini baada ya
mambo kwenda ndivyo sivyo,kwani angewalipa fedha mamluki hao pasipokuwa na
ushindi.
Aidha
upepo ulizidi kuwa mbaya kwao kwani walijikuta wasanii wao wakihamia upande wa
Emags na kuanza kuwashabikia mastaa wa filamu toka kampuni hiyo ya Emags na hata kuomba kupiga nao picha baada ya
mchezo jambo ambalo lilimkera bwana Isack na kugomea michezo siku nyingine
akidai kuwe na semina za sanaa si michezo kwani haina faida kwao kama kuigiza.
Hata
hivyo kila penye wengi hakukosi jambo kwani baada ya mchezo vijana hao
waliokuwa wamekodiwa walijikuta wakilipwa pesa chini ya makubaliano nakujikuta
wasanii wa osg wakichangishwa tena ili kuondoa aibu ambayo ingetokea mbele ya
kadamnasi iliyokuwepo jambo ambalo lilishuhudiwa na paparazzi wa blog hii.
Magoli
ya Emags yalifungwa na Maulidi (Mau) -2, Arnold(Dizo),-1 pamoja na kijana mrefu na machachari Aloyce
aliyefunga 1 pia,kwa upande wa OSG majina ya wafungaji yalishindikana
kupatikana kwania hata mkurugenzi wao hakuwajua majina.
Aidha
mchezo ulimalizika bila ugomvi na kufungwa na mkurugenzi wa kampuni ya Emags Bw:
Eliasi Magesa aliyetishia amani ya mabeki wa OSG kwa kuwalamba chenga sana na kupiga
mashuti makali yaliompa kipa wakati mgumu licha ya umri kuwa mkubwa.naye
aliitimisha kwa kuomba michezo iendelezwe ili kuleta urafiki mzuri na pia
wasanii kufahamiana ,lakini akiwaomba timu za makampuni ya uma na binafsi
,pamoja na wasanii wa Bongo movie kujipima kwa timu ya Emags kwani iko vema .
Emags ilianza vema kushiriki michezo
ilipoitililishia mvua za magoli timu ya Kings Entertainment ya mzee majuto
mjini Tanga magoli 9 kwa 2,radio 5 Arusha waliopata kipigo cha bao 6 kwa 1 na
OSG waliolazimisha sare kwa kucheza dakika 130 ili kusawazisha
PICHA ZA MATUKIO YA UWANJANI
|
CAMERAMAN DENNIS ALIKUA AKIFANYA YAKE |
|
BENCHI LA EMAGS WAKIWA WANASHANGILIA |
|
BENCHI LA UFUNDI LA OSG |
|
DIZZLE MAN DILLUNGA AKIPIGA PENALTI |
|
DEO G "GOALKEEPER WA EMAGS" |
|
BENCHI LA EMAGS WAKATI WA MAPUMZIKO |
|
BENCHI LA EMAGS WAKATI WA MAPUMZIKO |
|
EMAGS WAKIFANYA WARM UP KABLA YA MECHI |
|
MAPUMZIKO WACHEZAJI WAKIBADILISHANA MAWAZO |
|
RODGERS, DIZZLE NA MAURICE WAKISHANGILIA GOLI |
|
HEKA HEKA GOLINI MWA OSG |
|
WACHEZAJI WAKIRUDI UWANJANI KUCHEZA KIPINDI CHA PILI |
|
HEKA HEKA ZA UWANJANI |
|
OSG WAKIFANYA WARM UP KABLA YA MECHI |
|
IBRAHIM JAMAL AKIMPA GOALKEEPER DEO G MAZOEZI KABLA YA MECHI |
No comments:
Post a Comment