WASANII WANAHITAJIKA

EMAGS

Wednesday, February 6, 2013

ARUSHA MOVIE HAKUKALIKI


Lile shirikisho la filamu Jijini Arusha ambalo linasemekana liliundwa kiujanja ujanja na kupewa jina la ARUSHA MOVIE kwa sasa hakukaliki na hii ni baada ya tetesi zilizotufikia kuwa wanachama wa shirikisho hilo ambao pia ni viongozi wameanza kulogana.
Hayo yamebainishwa na mtoa taarifa wetu baada ya Katibu Mkuu wa shirikisho hilo la filamu Arusha (ARUSHA MOVIE) ndugu ISAACK ambaye pia ni mkurugenzi wa kikundi cha sanaa cha OSG, kulazwa katika hospitali ya mkoa ya Mount Meru huku akiwa amewekewa drip tisa ndani ya muda mchache na kwa majibu ya Daktari ni kwamba ugonjwa haukuonekana walipo mfanyia vipimo kwa mara ya kwanza.
Hata hivyo baadhi ya wasanii ambao ni wanachama wa ARUSHA MOVIE walipoulizwa juu ya sakata hilia walisema kuwa “Ni kweli mambo haya yapo ya kulogana kwani kumezuka hali ya sintofahamu kwa viongozi wetu huku wengine wakizushiana skendo, kiongozi mmoja jina kapuni inasemekana alifumaniwa na mke wa mtu”
Kwa upande wake ndugu ISAACK alipotafutwa kuzungumzia sakata hili yeye alisema kuwa “Ni kweli ndugu mwandishi nililazwa katika hospitali ya Mkoa ya Mount Meru kwa siku kadhaa na pia nilitundikiwa dripu takribani tisa, hiyo ni kutokana na kukutwa na ugonjwa wa malaria baada ya madaktari kuchukua vipimo kwa mara ya pili”
www.arushaprofessionalmovies.blogspot.com itaendelea kufuatilia sakata hili la ARUSHA MOVIE na kuwaletea habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment