WASANII WANAHITAJIKA

EMAGS

Monday, February 11, 2013

DAWA YA KWININI YATIBU UCHAWI UNAOENDELEA NDANI YA ARUSHA MOVIE


Baada ya  kashfa nzito ya ushirikina ndani ya wasanii wa Arusha  movie,kwa kile kilichodaiwa katika toleo la mwanzo la mtandao huu kurogwa kwa katibu wa klabu hiyo Bw.Isack ambaye pia ni mkurugenzi wa kikundi cha sanaa OSG jijini hapa ,katibu huyo amejitokeza hadharani na kuweka mambo wazi huku akidai kupona kwa dripu 9 za kwinini.
Hata hivyo akionesha kuwa fiti nakuanza majukumu yake kama katibu,alionekana katika kituo cha polisi mjini kati akiwa na jazba na kumburuza mwandishi  wa mswada wa filamu walio tarajia kuicheza ijulikanayo kwa jina la “the bodyguard of Queen”.

Mshtakiwa huyo aliyefahamika kwa jina la Charity Klavery alidaiwa kuwaraghai  wasanii wa kundi la OSG na wengine waliojitokeza kucheza filamu hiyo,huku akidai kuwa amepata ufadhiri  kutoka kwa mwanamuziki maarufu wa injili kutoka nchini Kenya  “jina tunalihifadhi”,na kuwafanyisha mazoezi kwa muda mrefu bila ya malipo akiwemo mjane wa mwanamuziki maarufu aliyewahi kutamba jijini Arusha na Afrika Mashariki kwa ujumla kwa nyimbo za kuabudu.

Hata hivyo mjane huyo alishtukia janja ya nyani ya Bw.Charity nakuamua kuachana nao baada ya kushindwa makubaliano ya malipo ya kucheza filamu hiyo kwani alipaswa kucheza kama muhusika mkuu yani  Malkia.
Mambo hayakukaa vema kwani Charity alishindwa hata kuleta mswada huo na kuamua kuleta muongozaji wa filamu  mwingine kutoka mjini Moshi aliyetambulika kwa jina la Ibra aliye wahi kusimamia filamu za msanii maarufu nchini kwa jina Ray ,ambaye aliwakataa wasanii waliokuwepo nakutaka wasanii wapya jambo lililosababisha mvutano kati yake na katibu Isack aliyekuwa msimamizi wa awali.

Aidha baada ya vuta ni kuvute hiyo,Isack aliamua kutumia nguvu za dora kupata haki za wasanii wake ,ndipo aliamua kumburuza Charity kituo cha polisi nakudai fidia kwa kupotezewa muda jambo lililokuwa gumu kwa upande wa Charity nakuamua kuwapa muswada wa filamu hiyo kama fidia jambo lililotekelezwa  mbele ya mwanasheria .

Hata hivyo licha ya kupewa muswada huo haijajulikana filamu hiyo itachezwa lini kwani hali ya uchumi bado ni tete.

No comments:

Post a Comment