MAUREEN / HAPPY |
Baada ya habari juu ya kuwaliza wenzake kutapakaa
,msanii Maureen alizama moja kwa moja katika ofisi za blog ya Arusha
professional nakudai kuwa hajawaliza wenzake wala si kweli kuwa anatembea na
big boss huyo wa utalii.
Akizungumza kwa jazba na mwandishi wetu, “kwanza
ndugu yangu nikwambie hao wanaosema juu yangu nikuwa wanataka kusafiria nyota
yangu hata sijatoka maskini,lakini mi nikuweke plain tu kuwa sina mahusiano
zaidi ya kuwa na urafiki tu wa kawaida na huyo kaka,mimi nina mchumba wangu
ambaye yuko Ufaransa hivyo hao lengo lao nikutaka kuniharibia tu.
Baada ya maelezo hayo akafunguka juu ya ugomvi wake
na msanii mwenzake anayetembea na pedeshee huyo akatililika “sina ugomvi na mtu
wala sina mda wakushea na mtu,kama yeye anasema nimemuingilia basi nimemuachia
aendelee nae mi nina mambo yangu na sina muda wakupoteza”.
Haikuishia hapo ,ghafla akaanza bonge ya vurugu na
mwandishi wa habari ya blog hii, “mi sitaki kuandikwa kwanini
mnifuatilie?mnajua nina tegemea ndugu zangu unazani wakiona nitawajibu kitu
gani ,mi nawaheshimu naomba na nyie mniheshimu”alinukuliwa akisema Maureen.
Aidha haikupita masaa kabla ya kutoka katika ofisi
zetu akabambwa tena akiteta na wasanii wenzake kuwa hivi karibuni lazima awe
star kupitia mtandao huu na kuwa alikuwa anazuga tu kugombana na mwandishi ila
ni ishu sana kuandikwa.
Hata hivyo blog hii haitasita kukuletea lolote
litakaloendelea katika baragumu hili la mastaa watarajiwa wa bongo movie lakini
tukiwahasa kutoendelea na tabia za bifu na mambo ya kashfa bali wazingatie
sanaa ili kuelimisha jamii kwani kashfa
si dilii nomaaaa….
No comments:
Post a Comment