Ashindwa kujifunga khanga,azitupia nakutia
wenzake aibu…
MSANII WA FILAMU ALIVYOFUNGA KANGHA MSIBANI KAMA ANAENDA BAFUNI |
Msanii
mwenye sura ya mauzo mnamo tasnia ya filamu
jijini Arusha aliyefahamika kwa jina moja la Jack almaarufu kama Baby
Face,amejikuta akiingiwa aibu ya mwaka alipoburuzwa na wenzake kwenda
kuhudhuria msiba wa mmoja wa wasanii wenzake aliyefiwa na baba yake mzazi
katika maeneo ya Sakina kitaa cha Silent Inn.
JACKY KATIKA POZI MSIBANI |
Bishosti
huyo alikubwa na balaa hilo pale alipokaribia maeneo ya msiba na kutoa khanga
zake kwaajili yakujistili nakutia fola baada ya kushindwa kujifunga na khanga
kumuanguka chini kila aliposogeza hatua moja,jambo lililowafanya wenzake
kusimama kwa dakika kadhaa wakimsaidia namna ya kujifunga ili waingie eneo la
msiba.
JACKY MAUZO |
Aidha
licha ya kusaidiwa alionekana kutokuwa mzoefu wa mitoko hiyo na kujifunga kama
mtu aendae bafuni akiacha kichwa wazi kilichokuwa na staili iliyowafanya
waombolezaji kumkodolea macho kwa muda mrefu wakimfananisha na msanii nguli Jackline
wolper huku wengine wakinong’ona kuwa ni mdogo wa Amber Rose huyo wa bongo.
AKIONEKANA MWENYE FURAHA MSIBANI BADALA YA HUZUNI |
Kuonesha
kutokujali msanii huyo alitupia headphones zake katika masikio na kuendelea
kula ngoma za kibongo nakujisahau kuwa alikuwa katika eneo la msiba na
kuwafanya wenzake kuinamisha vichwa kwa muda kukwepa aibu hiyo.
AKITAFAKARI NAMNA YA KUFUNGA KANGHA |
Hata
hivyo Arusha professional inamuomba kisura huyo kubadili mapigo nakujichanganya
katika mazingira yote kwani yeye ni kioo cha jamii na kuwaomba wasanii wengine
kutofautisha maisha yao yakisanaa na kisupastaa hata katika mambo yasiyofaa.
No comments:
Post a Comment