EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT YASAKA VIPAJI VIPYA
VYA WAIGIZAJI.
Kampuni
maarufu ya utengenezaji wa filamu jijini Arusha,ambayo imejizolea umaarufu
mkubwa baada ya kutoa filamu kadhaa ikiwemo “Mateka wa kiroho,Standard
7,tamthiliya ya Haiba ya penzi na kutengeneza kazi nyingine
kibao ikiwemo Nampenda motika,Chozi la yatima na mzigo unaotarajia
kudondoshwa sokoni na wasambazaji namba moja Steps uliobeba jina la Temptation
of my wife lakini pia wakitarajiwa kuwa na reality show kali inayokuja
hivi karibuni kupitia Tbc1 iitwayo “young millionea”.
|
DIRECTOR WA EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT AKIWA KAZINI |
Akizungumza
na Blog hii,mkurugenzi wa kampuni hiyo Bw:Elias Magesa amesema kuwa “lengo la
kampuni ya Emags nikukuza sanaa ya Tanzania,na tunamshukuru Mungu tumeweza
kufanikiwa kufanya kazi nyingi kama nilivyokuainishia ndungu mwandishi”.
|
DIRECTOR WA EMAGS NA WASANII WAKIWA LOCATION |
Akiendelea
kuzungumza na mwandishi wetu Bw.Elias Magesa aliendelea kusema kuwa kwa sasa
wametoa nafasi kwa vijana na watu wazima kuonesha vipaji vyao vya kuigiza kwani
kwa sasa wanaandaa tamthiliya itakayorushwa na televisheni maarufu hapa
nchini,na pia kuendeleza wimbi la kutoa filamu kwani kwa kuanza wanataka kupiga
filamu mpya ya Lost Orphans,hivyo wahi nafasi kwani waweza kuwa kinara.
|
WASANII WA EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT WAKIFANYA YAO |
Aidha
alitoa namba za simu kwa yeyote atakae kuwa tayari kujiunga na kampuni kuwa ni
0754-014227/0656-396025/0787-661199 na 0658-288054.
|
MAMBO YA LOCATION HAYA |
|
DIRECTOR WA EMAGS AKIFANYA MAMBO YAKE |
|
MOJA YA CAMERA ZINAZOTUMIKA NA KAMPUNI YA EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT |
|
HAPA KAZI TUUUUUUUUUU |
|
HAKUNA KUCHEKA KAZI TUUUUUUUUUUUUUU |
No comments:
Post a Comment