WASANII WANAHITAJIKA

EMAGS

Monday, February 18, 2013

WASANII WA EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT WAADHIMISHA SIKU YA WAPENDANAO NA WATOTO YATIMA




WAIGIZAJI WA FILAMU TOKA EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WATOTO WA KITUO CHA FARAJA ORPHANS CHILDREN HOME
Kwa kawaida siku ya wapendanao duniani huadhimishwa kila tarehe 14 mwezi February kila mwaka na siku hii  ni maalumu kwaajili ya watu wote wenye upendo.

Mara nyingi watu wengi wamekua wakiiadhimisha siku hii kwa kuwa karibu na wapenzi wao na wake zao na kusahau kuwa siku hii huwa ni maalumu kwaajili ya watu wote kama ndugu, jamaa na marafiki na zaidi ya yote kwenda kuwaona wenye shida mbalimbali kama wagonjwa, walemavu , wajane na yatima.

Kwa kuonesha kuwa siku hiyo ni maalumu kwaajili ya watu wote na sio wapenzi tu, waigizaji toka kampuni ya EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT waliweza kuonesha upendo wao kwa kuwatembelea watoto yatima katika kituo cha FARAJA ORPHANS CHILDREN HOME kilichopo Jijini Arusha eneo la SHANGARAI wilayani ARUMERU.

Waigizaji hao walipoenda kituoni hapo waliwapelekea watoto hao vitu mbalimbali kama madaftari, penseli, sabuni, vyakula,sukari  na vitu vingine mbalimbali na baadaye wakaenda kucheza mpira wa migumuu na watoto wa kituoni hapo kuonesha kuwa wanawapenda sana.

Watoto hao walifurahi sana kutembelewa na waigizaji hao wa kampuni ya EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT na kuomba kutembelewa tena siku za usoni na sio siku ya wapendanao tu bali wakati wowote wanakaribishwa.

BWANA FARAJA - MLEZI WA FARAJA ORPHANAGE CHILDREN HOME
 Hata hivyo Mlezi wa kituo hicho Bwana Faraja aliweza kuelezea  historia ya kituo hicho kwa kuanza kusema “Mimi niliamua kuanzisha kituo hiki kutokana na vipimo vya kitaalumu kuonesha kuwa mimi sina uwezo wa kupata mtoto yaani siwezi kuzaa, nikaamua kuadopt (kuasili)  watoto watatu, lakini baadaye wakapata ufadhili wakaenda kusoma nje ya nchi”

Bwana faraja aliendelea kusema kuwa “ baadaye pia niliweza kuadopt (kuasili) watoto wengine watatu, ndipo nilipopata ushauri kutoka serikalini kwamba kuna leo na kesho hivyo ni vyema nifungue kituo cha watoto yatima na kuweza kukisajili ili kijulikane kisheria”

Hizi ni baadhi za picha na matukio mbalimbali yaliyofanywa na waigizaji hao wa kampuni ya EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT walipoenda kutembelea kituo cha FARAJA ORPHANS CHILDREN HOME….

WASANII WA MAIGIZO TOKA EMAGS WAKIELEKEA KITUO CHA FARAJA
MSANII WA FILAMU TOKA EMAGS IBRAHIM JAMAL (KULIA) AKIWAVUSHA WATOTO KUELEKEA UWANJANI
RODGERS(KUSHOTO) , ANNA (KATIKATI) NA MWIJAGE (KULIA) PAMOJA NA WATOTO WA KITUO CHA FARAJA
PAULINE (ALIYEVAA T SHIRT NYEUPE) TOKA EMAGS AKIWA NA WATOTO WA KITUO CHA FARAJA
WAIGIZAJI WA FILAMU TOKA EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT NA WATOTO WA KITUO CHA FARAJA ORPHANS CHILDREN HOME
WAIGIZAJI WA FILAMU TOKA EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT NA WATOTO WA KITUO CHA FARAJA ORPHANS CHILDREN HOME
WAIGIZAJI WA FILAMU TOKA EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT NA WATOTO WA KITUO CHA FARAJA ORPHANS CHILDREN HOME
WAIGIZAJI WA FILAMU TOKA EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT NA WATOTO WA KITUO CHA FARAJA ORPHANS CHILDREN HOME
WAIGIZAJI WA FILAMU TOKA EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT WAKIFANYA DRAMA
WAIGIZAJI WA FILAMU TOKA EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT WAKIFANYA DRAMA

No comments:

Post a Comment