MASS B KAZINI |
Msanii
wa sanaa ya maigizo na ngoma kutoka kundi maarufu la AGESTA anayekuja kwa kasi
toka jijini Arusha na kutambulika kwa
jina moja la Silivia,amejikuta
akizima ndoto zake za sanaa katika umri
mdogo pamoja na ajira yake katika shirika moja la kutetea haki za watoto
lililoko mjini hapa pasipo kutarajia huku akiwaacha midomo wazi wasanii wenzake kwa tukio lililomkuta hivi
karibuni.
Bishosti
huyo anayekadiriwa kuwa na umri chini ya miaka 18 amejikuta katika aibu
yakufunga mwaka 2012 na kufungua mwaka huu wa 2013 kwa aibu ya namna yake baada ya kupewa mimba au kwa lugha nyepesi
“kuwekewa kitumbua chake mchanga” na msanii mwenza wa kundi hilo
ajulikanae kama Masanja almaarufu “ Mass
B”.
Hata
hivyo balaa lilizidi kumkumba bidada huyo kwani alijikuta akilea mimba hiyo
pasipo msaada wa Mass B aliyekuwa amekana kuhusika kwa ishu hiyo kwani anaye
mchumba anaye ishi jijini Mwanza na
alikuwa katika mipango ya ndoa.
Aidha
baada ya muda baadhi ya wasanii wakaribu na Mass B walitumia sanaa kumshawishi
kijana huyo,na mwisho wa siku kujitia kitanzi na kukiri kuwa muhusika wa zigo
hilo na kutoa huduma zote kwa binti huyo mdogo.
Haikuishia
hapo kwani jamaa aliomba ridhaa ya kuishi na Silivia kwa lengo la kutoa malezi
ya mimba ,naye mlezi wa binti huyo hakusita aliwapa ruksa na sasa wanaishi pamoja mitaa ya
Sakina.
Hata
hivyo mtandao huu unampongeza binti huyo kwa kujifungua salama mtoto wa kike,nakuomba
wasanii kuwa makini na kutimiza ndoto zao kwa faida ya sanaa ya Tanzania.
MASS B NA SILVIA |
No comments:
Post a Comment