EVERYBODY |
Habari
zilizotufikia katika dawati letu la habari za uhakika kuwa msanii mmoja maarufu
wa filamu hapa Jijini Arusha aliyetamba katika filamu tofauti tofauti
alizozicheza kama muhusika mkuu ambazo ni MATEKA WA KIROHO, STANDARD 7, CHOZI
LA YATIMA na mzigo mpya unaokuja toka STEPS ENTERTAINMENT uitwayo TEMPTETION OF
MY WIFE pamoja na tamthilia ya HAIBA YA PENZI ambazo zimetengenezwa hapa hapa jijini
Arusha na kampuni maarufu ya utengenezaji filamu EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT,
Habari
hizi zinasema kuwa msanii huyu inasadikika kuwa alitelekeza familia yake baada
ya kua na mahusiano na msanii mwenzake maarufu wa filamu hapa jijini Arusha.
COVER LA FILAMU YA MATEKA WA KIROHO |
Inasemekana
kuwa msanii huyo ambaye jina lake halisi ni JOSEPHAT HOREST na maarufu kwa jina
la EVERYBODY alimwache mke na mtoto {MAMA CATHY} na kuingia kwenye mahusiano na msanii
mwenzake MWANAHAMISI MZIRAY maarufu kama MISHI.
Mtoa
habari wetu aliendelea kusema kuwa mahusiano ya EVERYBODY na MISHI hayakudumu
kwa muda mrefu kwani alimpa kibuti na kuvuta kifaa kingine kipya toka kundi
moja la sanaa hapa jijini Arusha aitwaye NASRA ambaye kwa sasa ana mtoto na
haijulikani ni mtoto wa nani na kwa sasa msanii EVERYBODY amemlazimisha NASRA
kumuachisha mtoto kunyonya ili aendelee kuponda raha kama kawa.
COVER LA FILAMU YA STANDARD 7 |
Kwa
upande mwingine mwandishi wetu alimua kujikiingiza mtaani na kumtafuta mke wa
EVERYBODY ambaye ni MAMA CATHY na kupiga nae story mbili tatu juu ya sakata
hili ndipo yakazuka mengine ambayo tulikua hatuyafahamu ambayo ni
“Mimi
na mume wangu kwa kweli tuligombana baada ya yeye kuwa star wa filamu kwani
hapo nyuma tulikua tunaishi kwa amani hadi tulipofanikiwa kumpata mtoto wetu
huyu {akimwonyesha cathy}, kwa sasa hatuna mahusiano mazuri kwani kuna kipindi
tulifikishana mpaka USTAWI WA JAMII kwani yeye alikua haleti pesa ya matumizi
ya mtoto”
Baada
ya kupata habari hizi mwandishi wetu aliamua kumtafuta EVERYBODY lakini
hakupatikana na alipotafutwa kwenye simu nayo iliita pasipo kupokelewa.
www.arushaprofessionalmovies.blogspot.com itawaletea
interview maalumu na msanii EVERYBODY baada ya kumpata.
?????????????????????????? |
No comments:
Post a Comment