WASANII WANAHITAJIKA

EMAGS

Monday, February 18, 2013

WASANII WAGOMEA OFA YA KWENDA NCHINI INDIA


NDUGU AWADHI NGOMA MKURUGENZI - KUNDI LA SANAA LA WATOTO WA SIMBA

Kikundi cha sanaa cha ngoma na maigizo cha WATOTO WA SIMBA chenye makazi yake Jijini Arusha kimegomea ofa ya safari yao ya kwenda kufanya tamasha katika Jimbo la GOHA nchini INDIA.

Akizungumza na mwandishi wetu wa www.arushaprofessionalmovies.blogspot.com katika ofisi zetu ndugu AWADHI RAMADHANI MWINYI maarufu kwa jina la AWADHI NGOMA ambaye ni Mkurugenzi wa kundi hilo alisema kuwa “Tumeona tusiende kwenye tamasha hilo nchini INDIA kutokana na promota wetu kutupa maslahi madogo, ila tunashukuru baadhi ya wasanii wamepata passport za kusafiria ili ikitokea tena safari ya nje tunaweza kwenda bila usumbufu wowote”
NDUGU AWADHI AKIONGEA NA MHARIRI WETU KATIKA OFISI ZA ARUSHA PROFESSIONAL MOVIES
 Bwana AWADHI aliendelea kusema “Tulioneshwa barua ya mwaliko wa kufanya tamasha hilo ambapo ilikua tunatakiwa kulipwa dola 1200, lakini malipo hayo yalikua yanakatwa na sisi kubaki na dola 400 kwa mwezi na chakula cha jioni walikua wanajitegemea wenyewe”

Safari yao ya kwenda nchini INDIA ilikua waende tarehe 5 march na walikua wanakaa kwa muda wa miezi sita, na alitoa ushauri kwa mapromota kuwa “Mapromota wasipende kujifikiria wenyewe waweke mbele maslahi ya wasanii halafu ndio yao ifuate kwani kundi lao lina jumla ya wasanii nane”

No comments:

Post a Comment