www.arushaprofessionalmovies.blogspot.com kama
kawaida inafuatilia habari zinazowahusu wasanii wa filamu hapa Jijini Arusha..
Weekend
hii tuliingia mtaani na kukutana na malalamiko toka kwa wanadada wawili tofauti
wakiwalaumu wapenzi wao kuwasusa katika kusheherekea siku zao za kuzaliwa..
DEO G |
Hii
imetokea tarehe 3/2/2013 majira ya mchana ambapo Mtangazaji maarufu wa SIBUKA
TV ambaye ana host show ya MASHARIKI HITS HIGH REQUEST ndugu ARNOLD RWEYEMAMU
a.k.a DIZZO MAN DILUNGA pamoja na mpiga picha maarufu wa habari wa chombo cha
CLOUDS TV hapa Jijini Arusha DEOKGRATIUS KASSAMIA a.k.a DEO G ambao pia ni
wasanii wa filamu kwani walishawahi kucheza filamu nyingi ambazo ni MATEKA WA KIROHO
, CHOZI LA YATIMA na tamthilia kali ya HAIBA YA PENZI..
Wanaume
hawa inasemekana mnamo tarehe 3/2/2013 walionekana maeneo ya NGURDOTO wakiwa na
mademu wengine tofauti na wapenzi wao wanaofahamika,
Hayo
yalisemwa na wapenzi wa wanaume hao ambao ni DELPHINE NDOSSY pamoja na SOPHIA
JUSTINE waliyasema hayo baada ya kuandaa zawadi za kuwapa wapenzi wao na siku
ilipofika ya kusheherekea siku zao za kuzaliwa wapenzi wao hawakuonekana na
inasemekana walionekana maeneo ya ngurdoto wakijirusha na wanawake wengine.
Waliendelea
kusema kuwa “zawadi zetu tulizowanunulia ili kuwapa wapenzi wetu tuliamua
kuwapa ndugu, jamaa na marafiki kwani inaonekana kuwa wsisi hatuna thamani
mioyoni na maishani mwao”
DIZZO MAN DILUNGA |
Kwa
upande wao DIZZO MAN DILUNGA na DEO G wao pia walifunguka kuwa “siku hiyo kwa
kweli tulikua tuko Ngurdoto lakini hatukua na wasichana wala hatukujirusha ila
tulikua tunafuatilia habari kwani kulikua na mkutano wa viongozi wanchi
mbalimbali hivyo tuliamua kusheherekea siku hiyo tukiwa kazini”
Lakini
kwa habari za uhakika toka www.arushaprofessionalmovies.blogspot.com ni kuwa
siku hiyo ya Jumapili ya tarehe 3/2/2013 hakukua na kikao chochote hapo
Ngurdoto hivyo kuonekana kuwa ni kweli walikua wanajirusha na wapenzi wengine
na kuwaacha solemba wapenzi wao wanaofahamika na watu wote.
No comments:
Post a Comment