Lile sakata la kumpa msichana mdogo mwenye umri
chini ya miaka 18 laendelea kuibua mapya baada ya msanii anayedaiwa kufanya
unyama huo kuibuka na kukanusha vikali kuhusika na jambo hilo.
Msanii huyo ambaye alifika katika ofisi za Arusha
Professional Movies amekanusha vikali kwa kusema kilichoandikwa kililenga
kumchafulia jina na haiba yake katika jamii.
“Kilichoandikwa kililenga kunichafua na
kunidhalilisha” alisema msanii huyo huku akionekana mwenye jazba
Msanii huyo anayefahamika kwa jina la MASS B
anayedaiwa kuwa ni msanii katika kikundi cha sanaa cha AGESTA kilichopo Jijini
Arusha alikua ameambatana na baadhi ya viongozi wa kundi hilo, amesema katika
maisha yake hatarajii kutoka kwa njia ya skendo kama wasanii wengine.
“Mimi katika maisha yangu sitarajii kutoka kwa
skendo na ndio maana nafanya kazi zangu za sanaa kwa juhudi na kujituma”alisema
msanii huyo.
Aidha ameongeza kwamba hivi sasa yeye ameajiriwa na
shirika linaloshughulika na watoto hivyo kitendo cha kumuandika hivyo kinaweza
kuhatarisha kibarua chake na hivyo kumkosesha riziki.
“Kwa kweli sujafurahishwa na habari hizo kwani
zinaweza kuniharibia kibarua changu” alisema MASS B huku akiwa na sura ya
huzuni.
Hata hivyo msanii huyo aliweza kuthibitisha kuwa
alimpa binti huyo mimba lakini hana miaka chini ya kumi na nane kama
ilivyodaiwa hapo awali na kwa sasa wanaishi pamoja.
Aidha kwa upande wake kiongozi wa kundi hilo
aliyeambatana na msanii huyo aliyefahamika kwa jina moja la CHRISS alisema “Sisi AGESTA kwa sasa tumejiwekea
heshima mbele ya mkuu wa Mkoa pamoja na Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha, hivyo
tunaomba sana, kikundi chetu kisihusishwe kwa namna yeyote ile na masuala
binafsi ya msanii mmoja mmoja. Kikundi kisihusishwe kutokana na heshima yetu
kwa viongozi hao”
Arusha professional movies inawatakia kila la kheri
kundi hili la AGESTA katika kazi zao za sanaa.
No comments:
Post a Comment