Hiki
ni kipigo ambacho hakijawahi kutokea kwani wasanii wa filamu toka kampuni ya
EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT waliweza kuwachapa na kuwaadabisha hadharani bila
woga wowote mbele ya wasikilizaji wao wafanyakazi wa RADIO FIVE ARUSHA kwa
kuwafunga goli 6 kwa 1.
Mchezo
huo wa aina yake ulifanyika mwishoni mwa wiki katika uwanja wa GENERAL TYRE
Jijini Arusha ulishuhudia RADIO FIVE ARUSHA ikipokea kipigo heavy toka kwa
wasanii wa filamu wa kampuni ya EMAGS VIDEO ENTERTAINMENT.
Magoli
hayo yalifungwa na wachezaji tofauti.
wakiongozwa na team captain RODGERS
ISRAEL NELSON aliyefungua pazia la kufunga magoli kwa timu ya waigizaji wa
filamu mnamo dakika ya tatu tu ya
mchezo, goli la pili lilifungwa na IBRAHIM JAMAL kiungo mchezeshaji, goli la
tatu lilifungwa na winga machachari na mfupi kuliko wote ABBY CARTER, goli la
nne na la tano lilifungwa na mshambuliaji hatari asiyecheka na nyavu SEVERINUS
MWIJAGE Jr na goli la mwisho lilifungwa na kiungo mshambuliaji MAULIDI huku
RADIO FIVE ARUSHA wakijipatia bao lao la kufutia machozi dakika ya tisini ya
mchezo lililofungwa na MENEJA wa RADIO FIVE ARUSHA ndugu JIMMY.
Hata
hivyo baada ya kuchapwa magoli matatu ya mwanzo RADIO FIVE ARUSHA walianza
kulaumiana na mchezaji wao SEMIO SONYO alianza kugoma kucheza kwa madai ya
kutoelewana na mchezaji mwenzake lakini wachezaji wenzake wakasema ni kawaida
yake kwani ndivyo anavyotafuta sifa..
Mechi
yenyewe ilikua hivi………………..
No comments:
Post a Comment